Simba yawasili Arusha ikiifuata Singida BS Manyara

Simba yawasili Arusha ikiifuata Singida BS Manyara

Kikosi cha Simba kimewasili jijini Arusha, ambapo kitaweka kambi ya siku moja kabla ya kuendelea na safari ya kuelekea mkoani Manyara tayari kwa mchezo wa nusu fainali Kombe la FA dhidi ya Singida Black Stars.

Mchezo huo umepangwa kuchezwa keshokutwa Jumamosi, Mei 31 kwenye uwanja wa Tanzanite Kwaraa mjini Babati.

Tayari mabingwa watetezi wa michuano hiyo Yanga wameshatangulia fainali baada ya kuifunga JKT Tanzania 2-0.

Leave a Comment

Comments

No comments yet. Why don’t you start the discussion?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *