MAZUNGUMZO baina ya wakala wa mshambuliaji wa Manchester United anayecheza kwa mkopo Aston Villa, Marcus Rashford na Mkurugenzi wa Michezo Barcelona, Deco, yanadaiwa kwenda vizuri na kuna asilimia kadhaa za staa hiyo wa lkimataifa wa England kutua Nou Camp katika dirisha lijalo.
Vyombo vya habari mbalimbali vya Hispania, juzi viliripoti kuwa wakala huyo ametua Hispania kwa ajili ya mazungumzo.