Mshambuliaji Marcus Rashford afurahia kupunguziwa mshahara ili kupewa fursa ya kuhama Manchester United kwenda Barcelona, Arsenal wapania kumchukua Jakub Kiwior kutoka Napoli, AC Milan wakataa ofa ya Manchester City kwa Tijjani Reijnders.
Mshambulizi wa Manchester United na Muingereza Marcus Rashford, 27, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo Aston Villa, yuko tayari kupunguza mshahara wake ili kuhamia Barcelona msimu wa joto. (Mundo Deportivo – in Spanish)
Barcelona wanataka kumchukua Rashford kwa mkopo kutoka Manchester United mara ya kwanza lakini wakiwa na chaguo la kumnunua. (Sport – in Spanish)