Klabu ya Sunderland imepanda daraja kwenda Ligi Kuu England msimu ujao wa 2025/26 baada ya miaka 8 kufuatia ushindi wa 2-1 dhidi ya Sheffield United katika dimba la Wembley kwenye fainali ya ‘playoff’.
Sunderland imeungana na Leeds United na Burnley ambao pia wamepanda daraja wakichukua nafasi ya Leicester City, Ipswich Town na Southampton walioshuka daraja kwenda Ligi ya Championship, England.
FT: Sheffield United 1-2 Sunderland
⚽ 25’ Campbell
⚽ 76’ Mayenda
⚽ 90+5’ Watson