December 2, 2025

Shaffih Dauda “Tusimlaumu Kocha wa Simba Pantev Kufungwa Kwa Simba”

0


Pamoja na Simba kupoteza mchezo wa jana ambao ni mchezo wa pili mfululizo kwa hatua ya makundi , Meneja Dimitar Pantev amejitahidi sana kiuchezaji kwa kulinganisha na mchezo wa kwanza ambao mimi pia ni katoka waliomkosoa .

Nimejiridhisha kuwa Simba SC ndio timu iliyotengeneza nafasi nyingi zaidi kwa siku ya jana kwenye mechi zote za CAF [ CL & CC ]

Simba alikuwa na uwezo wa kupata mabao hadi 5 kama nafasi zote zingetumika ipasavyo
[ Ahoua , Mutale , Mutale , Mukwala + Maema ] nilizozisahau utaongeza hapo.

Kwenye mashindano ya CAF kupata nafasi za wazi ni jambo gumu sana ndio maaana mabao yanakuwa machache , lakini Simba ni timu iliyofanikiwa sana kwenye hilo , wana mwalimu ambaye tutamuhukumu kama timu haitengenezi nafasi lakini suala la kumalizia nafasi ni mchezaji binafsi na sio mwalimu.

Kama nilivyotoa lawama kwa mwalimu mechi ya kwanza , leo natoa pongezi kwa kubadilisha kitu kikosini japo wamekosa matokeo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *