BREAKING: Klabu ya ALAHLI Tripoli ya Libya Imetuma ofa ya Tsh 4.8 Bilion Kumsajili Fei Toto
BREAKING: Klabu ya ALAHLI Tripoli,ya Libya imetuma ofa ya $2,000,000 (tsh 4.8 bilion) ili kumsajili Fei Toto kutoka Azam Fc.
Klabu hiyo ya Libya imetuma ofa hiyo baada ya ile ya kwanza ($800,000) kukataliwa na Azam FC.
Tripoli wako tayari kulipa hela hiyo haraka sana ili kukamilisha dili hilo.
Pia Tripoli wako tayari kuweka kipengele cha Azam kupata 10% ya mauzo endapo Tripoli itamuuza Fei huko mbeleni.
Fei yuko tayari kuondoka Azam ili kutafuta maisha Libya
