Rabat, Morocco. Kocha Mkuu wa AS FAR ya Morocco, Alexandre Dos Santos amesema kuwa wanafanya maandalizi makubwa kwa ajili ya mechi yao ya kwanza ya hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Yanga itakayochezwa kwenye Uwanja wa New Amaan Complex Zanzibar, kati ya Novemba 21 hadi 23 mwaka huu.
Santos amesema kuwa sababu zinazowalazimisha kujipanga vilivyo kwa ajili ya mechi hiyo ni ubora na uzoefu mkubwa wa Yanga pamoja na lengo waliloweka la kuhakikisha wanapata ushindi katika michezo yote ya kundi hilo.
