Tue. Nov 4th, 2025

TIMU ya Wanawake ya JKT Queens imefanikiwa kutetea ubingwa wa Ngao ya Jamii 2025 kwa Wanawake kufuatia ushindi wa 2-1 dhidi ya Simba Queens kwenye fainali katika dimba la KMC Complex.

FT: JKT Queens 2-1 Simba Queens

⚽ 12’ Winfrida Gerald

⚽ 18’ Asha Omary (OG)

⚽ 90+4’ Zawadi Usanase

Kwenye mchezo wa mapema, Yanga Princes iliibuka na ushindi wa 3-0 dhidi ya Mashujaa Queens kwenye mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu.