Tue. Nov 4th, 2025

Klabu ya Azam Fc imetinga raundi ya pili ya kombe la Shirikisho Afrika (CAFCC) kufuatia ushindi wa jumla wa 4-0 dhidi ya EL Merriekh Bentiu ya Sudan Kusini Waoka mikate hao wakishinda 2-0 ugenini kabla ya kumaliza shughuli kwa ushindi wa 2-0 nyumbani Azam Complex, Chamazi.

Azam Fc watachuana na KMKM Fc ya Zanzibar kwenye raundi ya pili, KMKM ikifikia hatua hiyo kufuatia ushindi wa jumla wa 4-2, ushindi wa 2-1 ugenini kabla ya kushinda 2-1 nyumbani.

FT: Azam FC πŸ‡ΉπŸ‡Ώ 2-0 πŸ‡ΈπŸ‡Έ EL Merriekh Bentiu (Agg. 4-0)
⚽ 16’ Yoro
⚽ 90+3’ Saadun