Tue. Nov 4th, 2025

Anaandika @kelvinrabson_

✍️ Nafikiri Yanga SC wanatakiwa kuboresha zaidi hasa pale wasipokuwa na mpira , kuna nafasi kubwa kwenye maeneo yote matatu ilikuwa rahisi kwa Wiliete kuifikia defense ya yao kirahisi …. Kivipi ?

1: Wanakuwa wapo mbali mbali baina ya mchezaji mmoja na mwingi , hapo wakipoteza umiliki wa mpira ngumu kuurejesha .

2: Hata maamuzi yao yanakuwa sio sahihi ( Pass na movement )

3: Kunakuwa na ugumu wa kutengeneza connections kuanzia eneo la chini : Kuunganisha pasi zao kutokea eneo la chini .

✍️ Wakiwa na mpira wachezaji wa mbele wanaingia ndani kwenye “Half Spaces” wakiwa kwenye mstari mmoja na namba 10 ( Pacome , Maxi na Abuya ) wakati huo Fullbacks wanakuwa kama wingers .

✍️ Baada ya hapo Yanga wanakosa usahihi wa maamuzi yao ya mwisho : FBs wao cross zao hazikuwa nzuri , maamuzi yao ndani ya box hayakuwa sahihi then Ufanisi ulikuwa mdogo mbele ya goli .

✍️ Wiliete walianza vizuri mchezo sana , bila mpira wanakuwa na muundo mzuri wa kuzuia , utulivu wakati wanaanza build up na waliongeza usahihi wa pasi zao kusogea eneo la juu kirahisi : tatizo ni wakifika kwenye eneo la mbele ( walipoteza mipira kirahisi , walikosa Quality ya kuifungua defense ya Yanga walihitaji mchezaji mwenye uwezo wa kucheza kwenye maeneo finyu na kufanya vitu vitokee )

NOTE :

1: Aziz Andambwile anazidi kuimprove performance yake 👏 utulivu akiwa na mpira , usahihi wa pasi zake na nidhamu nzuri ya kuzuia nafasi .

2: Edmund John kacheza game nzuri sana ✅

3: Chikola zile cross zake 🙌 Kasi + nguvu kwenye mpira ( kacheza game nzuri )

4: Pacome anafanya vitu vitokee kwa urahisi 👏

5: Waliete walikosa QUALITY tu!.. walikuwa na game bora hasa kipindi cha kwanza .

6: BOKA anatakiwa kuboresha pasi zake za mwisho .

FT: Yanga SC 2-0 Wiliete ( Agg 5-0 )

Uchambuzi By : @kelvinrabson_