
Klabu ya Yanga SC imemtangaza Rashid Kalage kuwa Mwanasheria mpya wa klabu akichukua nafasi ya Simon Patrick
Hili limethinitishwa kupitia mkutano mkuu wa klabu ya Yanga unaofanyika September 7, 2025 ukumbi wa Superdome Masaki.
Ikumbukwe Rashid alikuwa ni mmoja kati ya mawakili waliokuwa wakiunda timu iliyofanikiwa kushinda kesi dhidi ya Mwanachama wa klabu hiyo, maarufu kama Mzee Magoma.