Wed. Nov 5th, 2025

Manchester United imetwaa ubingwa wa kombe la ‘Premier League Summer Series’ kufuatia sare ya 2-2 dhidi ya Everton katika dimba la Mercedes-Benz, Atlanta, Georgia Marekani.

Michuano hiyo ya maandalizi ya msimu mpya ilishirikisha timu nne za Ligi Kuu England Man United, West Ham United, Everton na Bournemouth ambapo Mashetani hao Wekundu wamemaliza kileleni pointi 7 baada ya mechi tatu, wakishinda mechi mbili na kutoka sare mechi moja.

FT: Man United 2-2 Everton
⚽ 18’ Bruno (P)
⚽ 69’ Mount

⚽ 40’ Ndiaye
⚽ 75’ Heaven (og

MSIMAMO:

  1. Man UTD — mechi 3 — pointi 7
  2. West Ham mechi 3 — pointi 6
  3. Bournemouth mechi 3 — pointi 3
  4. Everton mechi 3 — pointi 1