Wed. Nov 5th, 2025
Taifa Stars
Taifa Stars

Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) imetoka nyuma 1-0 na kushinda 2-1 dhidi ya Senegal kwenye mashindano ya CECAFA ya Mataifa matatu katika dimba la Black Rhinos, Karatu Tanzania.

Huu ni ushindi wa pili kwa Stars baada ya kuilaza Uganda The Cranes 1-0 kwenye mchezo wa kwanza wa mashindano hayo ambayo ni sehemu ya maandalizi ya michuano ya CHAN 2024 inayotarajiwa kuanza Agosti 2, 2025.

FT: Tanzania πŸ‡ΉπŸ‡Ώ 2-1 πŸ‡ΈπŸ‡³ Senegal
⚽ 53’ Sopu (P)
⚽ 56’ Bacca

⚽ 08’ Mbodji