Victor Osimhen anasimulia namna alivyomsaidia rafiki yake wa utotoni kiasi cha pesa lakini hakuonekana kukithamini.
Osimhen anasema: “Nilikuwa nikituma pesa kwa rafiki yangu mmoja wa utotoni, lakini siku moja, aliniambia kuhusu biashara anayotaka kuanzisha na alihitaji usaidizi wa kifedha. Nilimtumia €5k(zaidi ya Sh mil 13) lakini hakuithamini na hata akaniambia alisoma kwenye habari kwamba napokea mshahara euro milioni 1 kila wiki, na alitarajia kama ningempa euro 50k (zaidi ya Sh mil 130) kuanzisha biashara hii nilikasirika sana. Nilitaka kurudisha muamala lakini sikuweza.
“Pesa hizo €5k zinaweza tu kununua pea moja ya viatu huko Ulaya, lakini nchini Nigeria ni pesa nyingi. Hakuna aliyenitumia dola 1 kabla sijaja Ulaya, nilihangaika usiku na mchana, na niliuza maji ya chupa mitaani. Watu wanapaswa kujifunza kuthamini chochote wanachopata kama zawadi, wasiwe na hisia hii ya kustahiki.”
UNAMPA MAKSI NGAPI OSIMHEN?