TFF kuchunguza upangaji wa matokeo kwenye mechi hizi

Published from Blogger Prime Android App
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeutaarifu umma kuwa limepokea malalamiko ya kimaadili dhidi ya Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Tabora (TAREFA), Yusuph Kitumbo na Kocha Ulimboka Mwakingwe
Malalamiko hayo yanayohusisha madai ya upangaji matokeo yamewasilishwa na klabu ya Ligi ya Championship, Fountain Gate FC na tayari yamewasilishwa katika Kamati ya Maadili ya TFF ili yafanyiwe kazi kwa mujibu wa Kanuni za Maadili za TFF
Ili kulinda hadhi ya mpira wa miguu, TFF inawakumbusha wanafamilia wote wa mpira wa miguu kuwa itachukua hatua kali kwa yeyote atakayebainika kujihusisha na upangaji matokeo.
Leave a Comment

Comments

No comments yet. Why don’t you start the discussion?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *